AFYA YAKO KWANZA

JE UNATAKA USHAURI AU DAWA ZA ASILI PIGA 0763371047
Showing posts with label dawa asilia. Show all posts
Showing posts with label dawa asilia. Show all posts

Sunday, July 14, 2019

FAIDA MPYA YA MMEA WA MCHAICHAI

 Tokeo la picha la faida za majani ya chai

Ukitaka kuwafukuza Mbu wanaoleta ugonjwa wa Malaria nyumbani kwako panda Mmea wa Mchaichai au weka huo Mmea
ndani ya nyumba yako kama pambo basi Mbu hawata sogea nyumbani kwako utakuwa umewaweza Mbu wana uchukia huo Mmea wa Mchaichai. Haya nimewapeni Dawa ya bure hiyo kazi kwenu.
FAIDA YA KUTUMIA MCHAICHAI KAMA TIBA NA CHAKULA
Faida za mchachai zipo nyingi sana wengi wetu hudhani mchaichai ni kuongo cha kuweka kwenye chai pekee, au ni dawa kwa ajili ya kuua mbu pekee, ila mchaichai huwa na faida lukuki zaidi ya hizo tu. Naomba uweze kusoma makala haya ili uone faida nyinginezo za mchaichai.
Zifuatazo ni faida za kutumia mchaichai kiafya.
1. Mchaichai ni kinga dhidi ya saratani.
Tafiti mbalimbali zimeonyesha kuwa kwenye kila gram 100 ya mchaichai, kuna viondosha
sumu ambavyo vina uwezo wa kuukinda mwili dhidi ya ugonjwa wa saratani. Mwaka 2006, timu ya watafiti kutoka Chuo kikuu cha Gurion, Israel waligundua mchaichai una uwezo wa kuua seli zinaweza kusababisha saratani.
2. Hutibu magonjwa ya kuhara.
Husaidia umeng’enyaji wa chakula Chai ya mchaichai hurahisisha utaratibu wa mmeng’enyo wa chakula na pia hutibu magonjwa ya kuhara na maumivu ya tumbo ikiwamo kujaa gesi.
Hurahisisha utaratibu wa kuondoa uchafu mwilini Katika matibabu, unatibu magonjwa mengi ikiwemo kushusha joto, hasa kwa wagonjwa wanaosumbuliwa na malaria kali.
3. Husaidia kusafisha figo na mkojo.
Mchaichai pia una kazi ya kusafisha figo ambayo kazi yake kubwa ni kusafisha damu mwilini, kuondoa mafuta mabaya mwilini ambayo mengi yanatengenezwa na kemikali kiwandani na hivyo mwili kushindwa kuziondoa na baadaye kusasababisha magonjwa mbalimbali ikiwemo saratani.
Figo inapokuwa safi na imara, hata kazi nyingine kama kusafisha mkojo zinafanyika kirahisi kwani mkojo unapozidi kuwa mchafu mtu hujikuta akivimba mwili na wakati mwingine kufikia hata hatua ya kupoteza maisha.
4. Hupunguza maumivu wakati wa hedhi.
Mchaichai pia huwasaidia kina mama ambao wanaumwa na tumbo kipindi cha hedhi, ambao wengi wao huchukulia kama chango.
“Unapokunywa mchaichai, unawezesha kusafisha mirija ya uzazi na hivyo kuwezesha damu kupita kwa urahisi,”
5. Mchaichai hutibu vidonda vya tumbo na kupunguza kiwango cha gesi tumboni.
Hata hivyo kwa wagonjwa wanaosumbuliwa hasa na vidonda vya tumbo, mchaichai husaidia kuondoa gesi ambazo huwapata mara kwa mara.
Unachotakiwa kufanya ni ;
Kuendelea kutumia chai ambayo imepikwa kwa majani ya mchaichai mara kwa mara

ZIJUE FAIDA ZA MAJANI YA MPERA KWA AFYA YAKO BINAFSI

 Tokeo la picha la faida za majani ya mpera
Majani ya mpera yana faida kiafya kama tunda la pera. Majani ya mpera yana virutubisho vya kuzuia uvumbe na tannins zinafaida nyingi kiafya ikiwemo kutibu maumivu ya tumbo pamoja na ugonjwa au magonjwa ya kansa.

Faida ya majani ya mpera ni kama yafuatayo;

KUPUNGUZA MAFUTA MWILINI
- Matumizi ya majani ya mpera husaidia kupunguza kiwango cha madhara kwa binadamu. Matumizi ya majani ya mapera yanaweza kusaidia kuepuka matatizo ya magonjwa ya moyo na shinikizo la damu.

KUHARISHA
- Tafiti za kisayansi zimeonyesha kuwa kunywa chai ya majani ya mpera huweza kusaidia kukomesha tatizo la kuharisha

SARATANI YA TEZI DUME
- Majani ya mpera yana kiwango kikubwa cha Iycopene ambayo ni muhimu katika kupambana na saratani ya tezi dume kwa kuzuia uzalishaji wa homoni aina ya adrogen ambayo ni chanzo cha ukuaji wa chembe za saratani ya tezi dume

KUPUNGUZA UZITO
- Virutubisho vilivyoko kwenye jani la mpera husaidia kupunguza uzito kwa kuzuia wanga kuwa sukari ambapo mageuzo ya wanga kuwa sukari husababisha ongezeko la uzito kwenye mwili wa binadamu

Faida tano za kutumia Mlonge

 Tokeo la picha la faida za mlonge
Moringa maarufu kama Mlonge ni miongoni mwa miti muhimu kuliko yote duniani. Mti huu ukuao haraka hupandwa katika maeneo mengi na hutumika kama chakula cha binadamu, lishe ya mifugo, tiba mbadala na kusafisha maji.

Hizi ndiyo faida za mmea huo ambao unatibu maradhi mbalimbali:
1. Mti wa Mlonge husaidia watu walioathilika kiongeza cd4 cell (white blood cell) ndani ya mwili wa binadamu ambayo humsaidia mgonjwa kuondokana na miwasho katika damu na kuupa mwili nguvu na kuongeza hamu ya kula
2. Mti wa Mlonge hutibu maradhi sugu kama vile Kisukali (Kuimalisha na kurekebisha viwango ya sukari katika umri wa mwanadamu), Pressure, malaria, homa ya mara kwa mala, Saratani ya tumbo, hupunguza sonona stress, huleta hamu ya kunywa maji, jambo amabalo ni adimu kwa watu wengi pia huondoa uchovu mwili na kukufanya uwe na afya nzuli, mchangamfu na mwenye furaha
3. Majani na maua ya Moringa yanavirutubisho vingi kama vitamin A ( mara tatu zaidi ya karoti), Vitamini C (mara tatu zaidi ya ile ya machungwa), calcium (mara 140 zaidi ya ile inayopatikana katika maziwa ya gombe) na Potasiamu. Mmea huu umetumika kusadia udhibiti wa matatanisho yanayoletwa na ugonjwa wa ukimwi.
4. Faida nyingine itokanayo na unga wa majani ya mti wa mlonge ni kusafishia maji ambayo ni machafu na kuweza kuwa safi na salama na kuwa tayari kwa matumizi yoyote ya nyumbani kama vile kupikia na kunywa hii inaweza kuwa ni mbadala ya madawa mengine yanayoweza kutibu maji kama vile watergard na mengineyo.
5. Majani pia huweza kupakwa mwilini katika kutibu majipu na maambukizi ya ngozi. Waweza kutumia majani kama unavyotumia mchaichai na hapo unatibu homa. Majani ya Mlonge yanaweza kutafunwa mabichi, yaliyochemshwa kama mboga au yaliyokaushwa na kusagwa kuwa unga. Unga wake unaweza kuhifadhiwa kwa miezi kadhaa bila kupoteza ubora na faida zake za kiafya huku ukitumia kama kiungo kwenye mboga na mchuzi (zingatia usikaushe kwenye JUA)​Mafuta kutoka kwenye mbegu za mti wa Moringa huweza kutumika katika kupikia na kuwasha katika nyumba. Pia hutumika sana kwenye viwanda katika utengenazaji wa sabuni na bidhaa za urembo. Mafuta hukamuliwa kutoka kwenye mbegu kama ambavyo alizeti hukamuliwa.
Zipo faida nyingi za mmea huu ambao umegeuka kimbilio kwa wanaosumbuliwa na maradhi mbalimbali.